Monday 3 October 2016

ANGALIA MWILI WA FIRAUN-LANA TULLAH

FIRAUN LANATULLAH
HIKI NDICHO KILICHOMFANYA DR. MAURICE BUCAILLE ASILIMU : DR. Maurice bucaille ambaye alikuwa mwana sayansi mashuhuri Sana, yeye ndie aliyechaguliwa kwa ajili ya kufanya uchunguzi katika mwili wa firauni (pharaoh), ili ijulikane sababu ya kifo chake,  Kabla ya kufanya uchunguzi alikuwa mkiristo, na katika biblia imeelezwa kuwa firauni (pharaoh) hakuzamishwa na na bahari Bali alikufa kifo cha kawaida, lakini Dr. Maurice bucaille alipochunguza mwili wa firauni (pharaoh) alipata mchanga wa bahari katika mwili wake. Ambapo ilikuwa ushahidi uliodhaahiri kuwa firauni (pharaoh) alizamishwa na bahari,  Wakati wa uchunguzi Kuna mtu alimuambia kuwa katika kitabu cha waislamu kiitwacho Quran imeandikwa habari kuhusiana na firauni (pharaoh), (AL Quran 10:90-92) 90. Tukawavusha bahari Wana wa Israili, na Firauni na askari wake wakawafuatia kwa dhulma na uadui. Hata Firauni alipo kuwa anataka kuzama akasema: Naamini kuwa hapana mungu ila yule waliye muamini Wana wa Israili, na mimi ni miongoni mwa walio nyenyekea! 91. Ala! Sasa? Na hali uliasi kabla yake na ukawa miongoni mwa mafisadi! 92. Leo, basi, tutakuokoa kwa mwili wako, ili uwe Ishara kwa ajili ya walio nyuma yako. Na hakika watu wengi wameghafilika na Ishara zetu. Al Qur’an 10:90-92 Baada ya kusikia habari hii alishangaa Sana, akasema Quran ilikuja Baada ya miaka 2000 kupita tangu kifo cha firauni (pharaoh). Na mwili wake uligunduliwa 1898, na hakuna aliyemjua firauni kwa miaka 35000 kimakadirio,  Lakini Quran kumbe ishaeleza habari zake, na pia Quran imeelezea ishara Za firauni (pharaoh), leo ishara zote zimekubaliwa katika uchunguzi,  Na Baada ya Hilo ALHAMDULILLAH yeye akatangaza kuwa ni muislamu na kutoa shahada  ALLAH HU AKBAR
HIKI NDICHO KILICHOMFANYA DR. MAURICE BUCAILLE ASILIMU :
DR. Maurice bucaille ambaye alikuwa mwana sayansi mashuhuri Sana, yeye ndie aliyechaguliwa kwa ajili ya kufanya uchunguzi katika mwili wa firauni (pharaoh), ili ijulikane sababu ya kifo chake,
Kabla ya kufanya uchunguzi alikuwa mkiristo, na katika biblia imeelezwa kuwa firauni (pharaoh) hakuzamishwa na na bahari Bali alikufa kifo cha kawaida, lakini Dr. Maurice bucaille alipochunguza mwili wa firauni (pharaoh) alipata mchanga wa bahari katika mwili wake. Ambapo ilikuwa ushahidi uliodhaahiri kuwa firauni (pharaoh) alizamishwa na bahari,
Wakati wa uchunguzi Kuna mtu alimuambia kuwa katika kitabu cha waislamu kiitwacho Quran imeandikwa habari kuhusiana na firauni (pharaoh), (AL Quran 10:90-92)
90.
Tukawavusha bahari Wana wa Israili, na Firauni na askari wake wakawafuatia kwa dhulma na uadui. Hata Firauni alipo kuwa anataka kuzama akasema: Naamini kuwa hapana mungu ila yule waliye muamini Wana wa Israili, na mimi ni miongoni mwa walio nyenyekea!
91.
Ala! Sasa? Na hali uliasi kabla yake na ukawa miongoni mwa mafisadi!
92.
Leo, basi, tutakuokoa kwa mwili wako, ili uwe Ishara kwa ajili ya walio nyuma yako. Na hakika watu wengi wameghafilika na Ishara zetu.
Al Qur’an 10:90-92
Baada ya kusikia habari hii alishangaa Sana, akasema Quran ilikuja Baada ya miaka 2000 kupita tangu kifo cha firauni (pharaoh). Na mwili wake uligunduliwa 1898, na hakuna aliyemjua firauni kwa miaka 35000 kimakadirio,
Lakini Quran kumbe ishaeleza habari zake, na pia Quran imeelezea ishara Za firauni (pharaoh), leo ishara zote zimekubaliwa katika uchunguzi,
Na Baada ya Hilo ALHAMDULILLAH yeye akatangaza kuwa ni muislamu na kutoa shahada
ALLAH HU AKBAR

Saturday 1 October 2016

ULIMWENGU WA KIISLAMU, FURSA NA CHANGAMOTO


Assalamu alaikum ndugu Waislamu
hichi ni kijitabu kilichokusanya idadi ya makala kutoka Radio ya kiswahili ya Iran (kiswahili.irib.ir), na mkusanyaji wa makala hizi ni ndugu yenu Salim Al-Rajihiy, kwa hiyo haki za kunukuu au kuchapisha zimehifadhiwa na (kiswahili.irib.ir) Iran, na hakukua na malengo yeyote katika kuzikusanya makala hizi, isipokua ni kueneza fikra na utamaduni wa Kiislamu. Ahsanteni sana tusiache kuombeana dua.

Mwaka Mpya Wa Kiislamu Na Hukumu Ya Kusherehekea


Mwaka Mpya Wa Kiislamu Na Hukumu Ya Kusherehekea

Tunaingia kwenye mwaka mpya wa Kiislam (Hijriyyah). Je, vipi tuukaribishe mwaka huu wetu mpya? Na nini hukumu ya kusherehekea? Na nini umuhimu wa miezi ya Kiislamu?

Kuhesabika Mwaka Mpya
Miaka yetu ya Kiislam imeanza kuhesabika baada ya Nabiy (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  na Maswahaba kuhajiri (Hijrah) kutoka Makkah kwenda Madiynah. 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhu) akatoa ushauri kuwa kwa vile ni mara ya kwanza wanahamia katika mji ambao wataanza kutekeleza shariy’ah ya Kiislam, basi ni bora kuanza kuhesabu ya miaka kwa kuanzia mwezi huo waliohajiri, ambao ulikuwa ni mwezi wa Muharram.

Na pia inasemekana kuwa 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhu)  


Wednesday 24 August 2016

AL KAABA
 

IBADA YA HIJJA 

 UMRA

Nini Hijja?

Hijja, kilugha ni kukusudia; kisharia ni kukusudia kwenda Makka kutekeleza nguzo za Hija, tangu 'tawaf, sa'i (Safa na Marwa), kuhudhuria 'Arafa, na nguzo nyengine za Hija. Hutenda haya kutekeleza amri ya Mwenyezi Mungu Mtukufu na kutafuta ridhaa zake.

Hukmu ya Hijja


Hija ni fardhi kwa kila mwenye uwezo, ni nguzo ya tano miongoni mwa nguzo tano za Uislam. Hija imekuja kwa Qauli ya wenyezi Mungu Mtukufu, qauli ya Mtume wetu Mpenzi s.a.w. na itifaqi ya Umma. Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

 "............Na kwa ajili ya Mwenyezi Mungu imewajibikia watu wahiji kwenye Nyumba hiyo, kwa yule awezae njia ya kwendea……". (Al 'Imraan : 97).
Na amesema Mtume wetu Mpenzi s.a.w.:

 "Umejengwa Uislam juu ya (Nguzo) tano", (mpaka mwisho wa Hadithi).
Na amesema Mtume wetu Mpenzi s.a.w.:
  

 "Hijini kabla hamjakuwa hamuwezi kuhiji". (Imehadithiwa na Al Bayhaqy).
Mwenye kukanya kuwajibika Hija huwa amekufuru.


Tuesday 2 August 2016

TAASISI YA ISLAMIC SOCIAL SOLIDARITY PROGRESSIVE KWA KUSHIRIKIANA NA MEYA YA WILAYA YA TEMEKE WALIANDAA MASHINDANO YA QUR AN KATIKA KIPINDI CHA MWEZI MTUKUFU WA RAMADHANI MASHINDANO HAYO YALIHUSISHA WASHIRIKI WA JUZUU 3,5,7, PAMOJA NA JUZUU KUMI ZAWADI MBALIMBALI ZILITOLEWA KWA WASHINDI WA KWANZA ,PILI NA WATATU KATIKA KILA KUNDI

ZIFUATAZO NI VIDEO ZA BAADHI YA WASHIRIKI KATIKA MASHINDANO HAYO

 

YA PILI




Friday 3 April 2015

madhara ya bidaa katika uislamu

                                BIDAA NA VIPENGELE VYAKE
Baadhi ya vipengele vya Bid’ah ni kama vifuatavyo:

1. Kila bid’ah ni Dhwalaalah.
Kilugha Bid’ah ni kitu chochote kipya au kitu ambacho hakijafanywa kabla, yaani, hakina mfano kabisa wa mbeleni. Katika muono wa kisheria, kila Bid’ah ni Dhwalaalah na hakuna Bid’ah hasanah au sayyi’ah (Bid’ah nzuri na mbaya). Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema katika hadith, “Kullu Bid’atin dhwalaalah wa kullu dhwalaalatin fin naar (kila Bid’ah ni Dhwalaalah na kila Dhwalaalah ni motoni)” (Imepokewa na Imam Ahmad, Abu Dawud, at-Tirmidhy na wengineo).
Dhalalah ina maana ya kwenda kombo au kufuata njia ya upotevu na kwenda kinyume na ukweli. Tukitazama Qur-aan, tutaona vipi Allaah (Subhaanahu Wa Ta'ala) ametumia neno hilo ‘dhwalaalah’ au ‘dhwaal’. Neno hili linatumika kwa mtu anayefanya dhambi au anafanya kosa katika mambo ya kidini lakini na pia linatumika kwa wale watu ambao wamepotea kutoka kwa njia nyoofu au wale walioigawa dini. Kwa mfano katika Suratu Faatihah (Sura ya kwanza), neno lililotumika ni ‘Dhaaliin’ halikutumika kwa wafanyao madhambi pekee lakini limetumika kwa watu waliopotea kutoka kwa ile njia ya sawa, yaani Wakristo. Hivyo pale Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alipoielezea bid’ah, alitumia neno kali sana kwa upotevu huo, yaani dhalalah, kama alivyosema, “Kulla bid’atin dhwalaalah (kila bi’dah ni dhwalaalah)”. Hakusema kuwa kila bid’ah ni dhambi au ni kosa lakini kwa hakika ni jambo ambalo ni kubwa kuliko hilo. Huu ni upotevu, jambo ambalo linamtoa mtu katika Swiraatul Mustaqiym (njia ilinyooka).